Driver / Dereva

The School of St Judes logo The School of St Judes
Moshono Campus, Arusha, Tanzania
Full-Time
19th February 2026

Tangazo la Kazi: Nafasi ya Udereva (1)

Kuhusu Shule

Shule ya St Jude ni shule inayotoa elimu ya hisani ndani ya Tanzania. Shule hii inafadhiliwa na wafuasi wakarimu kutoka kote ulimwenguni, ambao huwezesha dhamira yetu ya kuwapa wanafunzi wa Kitanzania mahiri wanaotoka kwenye mazingira ya kimaskini elimu ya bure na yenye ubora wa hali ya juu.

Shule ya St Jude inayo furaha kutangaza nafasi moja (1) ya kazi ya Udereva kwa Watanzania wenye sifa stahiki.

Kazi na Majukumu

  • Kuendesha magari ya shule kwa uangalifu na umakini mkubwa.

  • Kukagua mara kwa mara gari ulilokabidhiwa ili kuhakikisha lipo salama kabla ya safari na wakati wa kuendesha.

  • Kutunza taarifa sahihi za gari, vipuri na matumizi ya mafuta, ikiwemo kujaza log book kwa usahihi kwa kila tukio na safari.

  • Kuripoti kwa wakati pale gari linapohitaji matengenezo au kwenda service.

  • Kufuata taratibu, sheria, kanuni na miongozo yote ya usalama barabarani.

  • Kutoa ushirikiano kwa mamlaka ya shule na taasisi husika pale linapotokea tatizo kwa gari la shule unaloendesha.

  • Kufuata mipangilio na ratiba za magari pamoja na maelekezo ya Dereva Mkuu kuhusu routes za magari.

  • Kushiriki sikukuu na shughuli za kijamii za Shule ya St Jude mara zitakapopangwa.

  • Kutoa taarifa ya maandishi endapo gari unaloendesha litapata hitilafu au ajali itakayozuia safari au ruti iliyopangwa kuendelea.

Sifa za Mwombaji

  • Awe Mtanzania mwenye umri usiopungua miaka 35.

  • Awe na uwezo mzuri wa kusoma na kuandika Kiswahili. Kuzungumza, kuandika au kusoma Kiingereza kutaboresha maombi.

  • Awe na leseni hai ya udereva ya daraja C-plain na HGV Class E, pamoja na vyeti husika.

  • Awe na cheti cha udereva kutoka chuo kinachotambulika.

  • Awe na uzoefu wa angalau miaka miwili (2) kuendesha mabasi ya shule pamoja na magari ya mizigo.

Vigezo na Masharti

Mwombaji anatakiwa kutimiza masharti yafuatayo kikamilifu kwa kuambatanisha:

  • Barua ya maombi ya kazi.

  • Wasifu binafsi (Curriculum Vitae – CV).

  • Barua ya uhakiki wa leseni kutoka Polisi.

  • Nakala ya cheti cha kuzaliwa.

  • Barua ya utambulisho kutoka kwa Mwenyekiti wa Mtaa anapoishi.

Kuambatanisha nyaraka au vyeti vya kughushi kutapelekea kuchukuliwa hatua za kisheria.

Maombi yawasilishwe binafsi katika Shule ya St Jude – Kampasi ya Moshono, kabla ya tarehe 19/02/2026.

Maombi yatakayowasilishwa baada ya tarehe na muda uliopangwa hayatafanyiwa kazi.

Tutawasiliana na waombaji watakaokidhi vigezo na sifa pekee kwa ajili ya majaribio na mahojiano.

ANGALIZO

TAFADHALI KUWA MAKINI NA MATENDO YA UDANGANYIFU KATIKA MATANGAZO YA KAZI NA MCHAKATO WA AJIRA. SHULE YA ST JUDE HAIOMBI MALIPO KATIKA HATUA YOYOTE YA MCHAKATO WA KUAJIRI. OMBI LOLLOTE LA MALIPO LIKATALIWE NA KURIPOTIWA KWA MAMLAKA YA UTEKELEZAJI WA SHERIA ZA MITAA KWA HATUA STAHIKI.

Application
Login to Quickly Apply