Karani wa Fedha Lulu Saccos Ltd Mbeya
Full-Time
18th July 2018

Bodi ya chama cha ushirika wa akiba na mikopo Lulu(Lulu Saccos Ltd) MBR.737 kilichopo Jiji la Mbeaya maeneo ya Soweto kata ya Ruanda kinatoa tangazo la kazi kwa nafasi zifuatazo:-

Karani wa Fedha - Nafasi 1

Sifa

  • Awe na umri kuanzia miaka 23 hadi 35
  • Awe na Elimu ya sekondari
  • Awe na stashahada ya uhasibu, ushirika na fedha ktuoka vyuo vinavyotambuliwa na Serikali
  • Awe ni mtanzania anayeishi katika jiji la Mbeya
  • Awe hajawahi kupatikana na kosa la jinai
  • Awe ni mtu wa kujituma
  • Awe ni mtu anayejisimamia mwenyewe
  • Awe anajua kutumia kompyuta
  • Awe ni mzaliwa wa mkoa wa Mbeya

Kazi

  • Kutunza na kuangalia wakati wote kasiki la chama
  • Kutunza vitaby vya fedha
  • Kupokea fedha taslimu
  • Kulipa malipo mbalimbali
  • Kufanya malinganisho ya fedha ya kila siku kwa kushirikiana na mhasibu msaidizi
  • Kuhakiki hati za benki kabla ya kukatia stakabadhi
  • Atafanya kazi zingine zozote atakazopangiwa na mwajiri wake
  • Kuandaa taarifa za fedha za kila siku
  • Awe ni mzaliwa wa mkoa wa Mbeya

KAZI HII NI YA KUJITOLEA KWA MUDA WA MIEZI MITANO(5) BAADA YA HAPO ATAAJIRIWA KAMA ATAKUWA AMEKIDHI VIGEZO

Utaratibu wa kuomba

  1. Mwombaji anatakiwa kuambatanisha picha mbili passport size
  2. Mwombaji atatakiwa kuambatanisha vivuli vya vyeti vya kuzaliwa na vya masomo
  3. Mwombaji aambatanishe CV yake wakati wa kuomba kazi
  4. Mwombaji aonyeshe mawasiliano yake bayana
  5. Mwombaji atakayefaulu kwa awamu ya kwanza ataitwa kwenye usaili
  6. Mwombaji atakeyeitwa kwenye usaili aje na vyeti halisi siku ya usaili
  7. Mwombaji atajigharamia mwenyewe wakati wa usaili
  8. Maombi yatumwe kwa:-

MWENYEKITI WA BODI

CHAMA CHA USHIRIKA WA AKIBA NA MIKOPO LULU

S.L.P 3467

MBEYA

Application

Sorry, this job no longer accepts new applications.